![]() View Full-Size Image |
Kichocheo cha Fasihi |
|
| ( Focus Publishers ) |
||
|
ksh 460.00
|
|
|
Mwandishi: K Wamitila ISBN: 9966-882-73-1 Kichocheo cha Fasihi: Simulizi na Andishi ni kitabu kilichoandikwa kwa mtindo mwepesi na rahisi kusomeka. Kitabu hiki kinachunguza vipengele vya kimsingi vya fasihi simulizi na fasihi andishi kwa undani unaopatikana kwa nadra sana katika vitabu vilivyochapishwa. Je,Kuna tofauti gani kati ya fasihi simulizi na andishi? Je, ni zipi tanzu kuu za fasihi simulizi? Je, ngomezi ni nini? Je, zipi tanzu kuu za fasihi andishi? Je. kuna tofauti gani kati ya fani ya maudhui, dhamira na maudhui. ujumbe na falsafa? Haya ni baadhi ya maswali yanayojibiwa kwa njia ya Kuvutia na inayoeleweka vizuri sana. Mtindo wa Kichocheo cha Fasihi, pamoja na undani wake, unalifanya somo la fasihi kuwa na mvuto mkubwa na kuweza kueleweka vyema kuliko ilivyokuwa kabla. Ni kitabu cha lazima kwa wanafunzi na waalimu katika shule za upili, vyuo vya ualimu na vyuo vikuu. Dkt. K, W. Wamitila ni mhadhiri mkuu anayefundisha somo la Nadharia na Fasihi ya Kiswahili katika Chuo cha Elimu na Masomo ya Mbali (Kikuyu), Chuo Kikuu cha Nairobi. Baadhi ya vitabu vyake ni Uhakiki wa Fasihi; Misingi na Vipengele vyake, Bina-Adamu! Zimwi la Leo (riwaya ya watoto) na English-Kiswahili Assorted Dictionary (na Florence M. Kyallo), vitabu vingine vitakavyochapishwa hivi karibuni ni; Kamusi Fasihi, Simba Mwamba na Safari ya Ajabu na Kovu la jana.
|
||
|
|
||
Customer Reviews:There are yet no reviews for this product.Please log in to write a review. |
||
| |
||
| |
||
List All Products |
|
|
Advanced Search |
|
| Lost Password? | |
| Forgot your username? | |
| No account yet? Register | |
|
|
|
| Download Area |